Faida za Ukombozi.

Teaching Legacy Letter
*First Published: 2014
*Last Updated: Februari 2026
15 min read
Je! Mungu ametengeneza njia ya kutuokoa kutoka kwa utumwa wa ufalme wa giza ili kuwa warithi wa ufalme wa nuru? Ndio ametengeneza. Njia ambayo Mungu ametufanyia ni kupitia kifo cha Yesu Kristo kwa niaba yetu. Msalabani, Yesu alichukua laana inayotokana nasi kwa uasi wetu, ili, sisi pia, tupate kuingia katika baraka ambazo Yesu alipata kwa utiifu wake. Baraka hizi hushughulikia eneo lote la ufalme wa nuru. Laana na baraka zote zimetekelezwa katika sehemu kuu tatu za maisha yetu: kiroho, kimwili na kiuchumi.
Faida za Kiroho.
Je! Ni laana gani za kiroho ambazo Kristo ametukomboa? Vivyo hivyo, ni baraka gani za kiroho ambazo Kristo ametupatia?
Kwanza kabisa, tuangalie sababu za msingi zinazoleta baraka na sababu zinazoleta laana.
Kama ukimtii Bwana Mungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii, Bwana Mungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia. Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtii Bwana Mungu wako. (Kumbukumbu la Torati 28: 1-2)
Kisha, Musa anaeleza kwanini laana hizo zinakuja.
Hata hivyo, kama hutamtii Bwana Mungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata. (Mstari wa 15)
Ni muhimu sana kwetu kuelewa tofauti kuu kati ya kupokea baraka na kupokea laana. Tofauti hiyo imeelezwa, katika kifungu kifupi lakini cha muhimu sana: “Sikiliza sauti ya BWANA Mungu wako.”
Hatma yetu wote kwa ustawi au kwa janga huamuliwa na sauti tunayosikiliza. Kusikiliza sauti ya Bwana na kutii kile Yeye Anasema kutaleta baraka. Lakini kutosikiliza sauti ya Bwana kunaleta laana nyingi. Haitoshi kusikiliza sauti ya Bwana tu lazima sisi pia tunatii kile anasema. Kwa upande mwingine, haiwezekani kutii kile Mungu anasema isipokuwa sisi kwanza kusikia sauti Yake, kwa sababu sauti yake inatuambia kile anachotaka tufanye.
Hatari kubwa ya kiroho ambayo inayowakabili wanaodai kuwa Wakristo ni kutojali sauti ya Mungu. Wengi wanaweza kuendelea katika shughuli zao za kidini na majukumu yao, ambayo ni ya kawaida na rasmi (mtindo wa maisha ambao wamekuza) bado bila ufahamu wowote wa sauti ya Mungu unaoendelea. Katika nyakati zote, hitaji moja ambalo Mungu anauliza kwa watu wake ni kwamba tusikilize sauti yake.
Biblia Inasema.
Sharti hili limesemwa wazi na Bwana mwenyewe ndani ya Yeremia 7: 22-23. Katika aya hizi, Mungu anafafanua kile Yeye alihitaji kwa Israeli.
Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu, lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
Tazama hitaji rahisi la Bwana kuwa Mungu wetu na sisi watu wake: “Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu.”
Unaweza kufikiria kuwa Agano Jipya ni tofauti, lakini hiyo sio kweli. Kanuni hiyo ni sawa kabisa. Yesu anaelezea katika mstari mmoja: “Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata”Yohana 10:27
Alama ambayo sisi kweli ni wa Yesu sio kwamba tunatumia mifumo fulani ya maisha ya dhehebu au ibada, lakini ni kwamba tunasikia sauti yake na, tukisikia sauti yake, kwamba tunamfuata. Njia rahisi ya baraka za Mungu ni kusikia na kutii sauti yake. Mwisho usioweza kuepukika wa kutosikia na kutii sauti ya Mungu ni kupokea laana.
Sasa nitaorodhesha kwa kifupi laana za eneo la kiroho la utu wetu zinazotokana na kutotii Mungu. Hizi zimeorodheshwa na Musa katika Kumbukumbu la Torati 28.
- Katika aya ya 20, Musa anasema tutapata fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu tunachokigusa kwa mkono katika yote tunayofanya.
- Katika aya ya 28, atakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili.
- Katika aya ya 34, Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu
- Katika aya ya 65, macho yaliyochoka kwa kungojea na moyo uliokata tamaa
Haya ni baadhi ya matokeo ya kirohotunayokutana nayo katika maisha ya watu katika ulimwengu wa leo: Kufadhaika, kuchanganyikiwa, uchungu wa ndani na mateso.
Je! Ni baraka gani katika ulimwengu wa kiroho ambazo hutokana na kutii? Kwa kweli, kuna baraka nyingi. Lakini ninaamini zinaweza kufupishwa kwa neno moja fupi na zuri: amani.
Wakati Isaya aliandika juu ya ubadilishanaji uliofanyika wakati Yesu alikufa msalabani, alisema hivi, “Adhabu iliyotuletea amani ilikuwa juu yake”. (Isaya 53:5) Yesu alivumilia hukumu na adhabu kwa sababu ya dhambi na kutotii kwetu ili tupatanishwe na Mungu. Kama matokeo ya kupatanishwa na Mungu, tunaweza kukombolewa kutoka kwa maumivu ya ndani, mateso, kuchanganyikiwa na kufadhaishwa. Tunaweza kujua ukweli wa amani ya moyoni.
Tutazame Maandiko mengine mawili katika Agano Jipya ambayo yanazungumza juu ya amani hii.
Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. (Warumi 5:1)
Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. Wafilipi 4:7
Manenomazurisana! Hatuna hatiatena. Hatuogopi tena kwamba kwa namna fulani hatumpendezi Mungu. Tuna amani na Mungu. Mstari huu mzuri katika Wafilipi 4 unaelezea matokeo ya uzoefu ndani yetu. Amani ya Mungu italinda mioyo na akili zetu katika ustaarabu wetu wa kisasa.
Katika muundo wake wa Kiebrania, neno amani linamaanisha zaidi ya kukosekana kwa mizozo. Inamaanisha ukamilifu au ustawi. Aina hii ya amani huanza ndani ya mtu wa ndani, lakini husababisha ustawi kamili. Inaathiri kila eneo la maisha yetu.
Faida za Kimwili.
Hebu sasa turudi kwenye Kumbukumbu la Torati 28 ili tuangalie laana zote za mwili zinazotokana na kutosikia na kutotii sauti ya Bwana. Kwa kweli ni nyingi. Unaposoma hili, kumbuka kuwa magonjwa haya yote yanasemwa kama laana ambazo sio za watu wa Mungu waliokombolewa.
Magonjwa yanakuangamiza (aya ya 21); magonjwa ya kudhoofisha, homa na kuwashwa (aya ya 22); majipu, vidonda, upele, na kuwashwa (aya ya 27); upofu (aya ya 28); majipu yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini. (aya ya 35).
Wengi wetu kama Wakristo tunavumilia laana wakati tunapaswa kufurahiya baraka. Kwa nini? Labda kwa sababu kuu mbili: labda kwa sababu hatujui kuwa hizo ni laana au kwa sababu hatutambui kwamba Yesu alitukomboa kutoka kwa laana ili tupate kurithi baraka. Tafadhali soma aya ya 59 ya Kumbukumbu la Torati 28 na uangalie ikiwa unaishi katika laana au baraka.
Bwana ataleta mapigo ya kutisha juu yako na kwa wazao wako, maafa makali na ya kudumu, magonjwa mazito na ya kudumu.
Taswira Dhahiri.
Nabii Isaya anatupatia taswira dhahiri kabisa ya matokeo ya kutotii na uasi. Akiongea na taifa la Israeli, analinganisha hali yao inayotokana na kutotii na ile ya mwili wenye ugonjwa:
Kwa nini mzidi kupigwa? Kwa nini kudumu katika uasi? Kichwa chako chote kimejeruhiwa, moyo wako wote ni mgonjwa. Kutoka wayo wako wa mguu hadi kwenye utosi wa kichwa chako hakuna uzima: ni majeraha matupu na makovu na vidonda vitokavyo damu, havikusafishwa au kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta. (Isaya 1:5-6)
Kifungu hiki ni picha ya sitiari ya matokeo ya kutotii.lakini, siku moja nilipokuwa nikisoma, Roho Mtakatifu alinionyeshea kitu kizuri na cha kupendeza. Niligundua kuwa Yesu alikuwa tayari amechukua laana zote juu Yake kwa sababu alikuwa mbadala wetu. Mistari hiyo haikuwa tu picha ya sitiari ya hali ya Israeli kama matokeo ya kutotii kwao. Zilikuwa pia picha halisi za Yesu akiwa ameangikwa msalabani.
Yesu alipigwa kwa mijeledi ya Kirumi, na nyuzi zake tisa za kutisha. Kichwa chake kilijeruhiwa: miiba ilishindiliwa kichwani mwake. Moyo wake wote uliteseka. Ninaamini Yesu alifariki kwa moyo uliovunjika. Kifungu hiki ni maelezo haswa juu ya Yesu alipokuwa akining’inia msalabani. Kwa nini alifanya hivyo? Kutukomboa kutoka kwa laana kwa kufanywa laana kwa ajili yetu. Laana hizo zote za mwili zilizotokana na uasi wetu dhidi ya Mungu zilimjia Yesu alipokuwa ameangikwa pale msalabani. Tuangalie sasa baraka za kimwili ambazo zilinunuliwa kwa ajili yetu na Yesu.
Tutatazama tena, kwanza kabisa, katika Isaya 53: 4-5:
Hakika alichukua udhaifu wetu na akajitwika huzuni zetu, hata hivyo tulidhania kuwa amepigwa na Mungu, akapigwa sana naye, na kuteswa. Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu, alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu; adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake, na kwa majeraha yake sisi tumepona.
Yesu alichukua matokeo ya mwili ya kutotii ili sisi pia tupate uponyaji. Tunaona hili katika kifungu hicho mwishoni mwa mstari wa 5, “Kwa vidonda vyake tumepona.” Kihalisi zaidi kwa Kiebrania inasema, “Kwa vidonda vyake uponyaji ulipatikana kwa ajili yetu.” Au labda tunaweza kusema, Uponyaji ulifanywa urithi wetu kupitia majeraha ambayo Yesu alipata kwenye mwili wake.
Sehemu inayofuata ya kifungu hiki imenukuliwa katika Agano Jipya katika injili ya Mathayo, ikielezea huduma ya Yesu katika kuponya wagonjwa na kutoa pepo wabaya. Hivi ndivyo inasema:
Jioni ile, wakamletea watu wengi waliopagawa na pepo wachafu, naye akawatoa wale pepo wachafu kwa neno lake, na kuwaponya wagonjwa wote. Haya yalifanyika ili litimie lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba: “Mwenyewe alitwaa udhaifu wetu na alichukua magonjwa yetu.” Mathayo 8:16-17
Mathayo hakuwa na shaka ni nani aliyetajwa katika Isaya 53. Aliweka dhahiri kuwa ni Yesu. Tazama pia kwamba Mathayo (ambaye alikuwa Myahudi na alielewa Kiebrania), hakuwa na shaka kwamba utekelezwaji wa aya hizo katika Isaya 53 ulikuwa wa kimwili. Ulikuwa uponyaji wa mwili wa wagonjwa ambao ulikuwa utimilifu wa unabii uliotolewa katika Isaya.
Angalia kile Yesu anasema katika kujibu wakosoaji wake kwa kumponya mtu siku ya Sabato:
Ikiwa mtoto aweza kutahiriwa siku ya Sabato kusudi sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumponya mtu mwili wake wote siku ya Sabato? Yohana 7:23
Yesu anamponya mtu kikamilifu. Kila eneo la mwanadamu na utu wa kibinadamu linaweza kuponywa kupitia Yesu.
Angalia pia kile Petro alisema baada ya uponyaji wa kiwete katika Lango nje ya hekalu liitwalo zuri katika Matendo 3:16. Hivi ndivyo alivyoelezea uponyaji:
Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona. Matendo 3:16
Matokeo yake ni nini? “Uponyaji kamili.” Yesu alisema, “Nimemponya mtu kikamilifu.” Huo ndio utendakazi wa kimwili wa ukombozi tuliopewa na Yesu. Tunashukuru kwa kazi ya madaktari, wataalamu wa magonjwa ya akili na wengine. Lakini kuna mtu mmoja tu katika ulimwengu anayeweza kusema, “Namponya mtu kikamilifu! Ninaweza kushughulikia shida zake zote: kiroho, kiakili, kihisia, na kimwili. “ Mtu huyo ni nani? Bwana Yesu Kristo.
Tunapowasiliana na Yesu kwa imani kwa msingi wa ukombozi wake, matokeo yale yale yaliyotokea na yaliyoandikwa katika Agano Jipya yanapatikana kwa ajili yako na mimi leo kwa njia ya imani katika Yesu.
Faida Za Kiuchumi
Sasa tutaangalia baraka na laana haswa katika eneo la uchumi Kwanza kabisa, tunaangalia baraka za kiuchumi zilizoahidiwa kwa kutii na ziko nyingi kweli kweli. (Haiwezekani kwangu katika barua hii fupi kuziorodhesha zote.) Hivi ndivyo Musa anasema katika Kumbukumbu la Torati 28
- Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani (aya ya 3)
- Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ng'ombe, na wana-kondoo wa makundi yako. (aya ya 4)
- Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa. (aya ya 5)
- Bwana ataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako. Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi anayokupa. (aya ya 8)
- Bwana atakupa kustawi kwa wingi, katika tunda la uzao wa tumbo lako, katika wanyama wachanga wa mifugo yako na katika mazao ya ardhi yako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwapa. (aya ya 11)
Maneno, “Bwana atakupa kustawi kwa wingi “yanaelezea baraka zinazotokana na kusikia na kutii sauti ya Bwana. Musa anarudi kwa kifupi kwenye mada hiyo hiyo katika Kumbukumbu la Torati 29: 9:
Fuateni kwa bidii masharti ya Agano hili, ili kwamba mweze kustawi katika kila kitu mnachofanya.
Kuzingatia maneno ya agano la Mungu kunasababisha sisi kufanikiwa katika yote tunayofanya. Hiyo haitoi nafasi ya kushindwa au kuchanganyikiwa katika eneo lolote la maisha yetu. Hizi ndizo baraka zilizoahidiwa kwa kutii.
Sasa tuangalie laana za kiuchumi kutokana na kutotii. Tukirudi kwenye Kumbukumbu la Torati 28:29, tunasoma:
Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huku na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lolote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyang'anywa, wala hakuna yeyote atakayekuokoa.
Kama vile kustawi kwa wingi ni baraka, kwa hivyo kutofanikiwa katika njia zetu ni laana. Kwa ukamilifu zaidi na wazi, Musa anasema hivi tena katika Kumbukumbu la Torati 28: 47-48. Hapa baraka na laana zimewekwa sambamba moja kwa moja.
Kwa sababu hukumtumikia Bwana Mungu wako kwa furaha na kwa moyo wakati wa kufanikiwa kwako, kwa hiyo katika njaa na kiu, katika uchi na umaskini wa kutisha, utawatumikia adui ambao Bwana atawatuma dhidi yako. Yeye ataweka nira ya chuma shingoni mwako hadi amekwisha kukuangamiza.
Hungeweza kuwa na njia mbadala mbili zilizo wazi zaidi kuliko katika aya hizo mbili. Matokeo ya kutii: wingi wa vitu vyote, kumtumikia Mungu kwa furaha na moyo wenye furaha. Matokeo ya kutotii: kutumikia maadui kwa njaa, kiu, uchi, na umaskini wa kutisha.
Wakati nilikuwa nikitafakari juu ya maneno hayo siku moja, niliona kuwa haya ni maelezo ya umaskini wa kutisha. Mtu ambaye ana njaa, hana chochote cha kula; ana kiu, hana kitu cha kunywa;Yuko uchi, hakuna nguo za kuvaa; na anakosa vitu vyote. Mtu huyo yuko katika hali ya umaskini kabisa. Haiwezekani kufikiria umaskini wa hali ya juu kuliko huo: njaa, kiu, uchi, na ukosefu wa vitu vyote. Ukweli muhimu tunahitaji kuona ni kwamba umaskini ni laana. Sio wa watu wa Mungu. Furaha na kufunguliwa vilikuja katika nafsi yangu wakati niliona hili wazi siku moja: umaskini sio wa watoto wa Mungu. Sio wa watu wa Mungu waliokombolewa. Badala yake, mapenzi ya Mungu ni wingi ili tumtumikie yeye kwa furaha na furaha ya moyo.
Wakati mmoja, nilikuwa nikihubiri katika mkutano huko New Zealand, Roho Mtakatifu wakati huo huo alikuwa akinionyeshea kitu katika roho yangu na akili yangu ambacho kimebaki nami tangu wakati huo. Roho Mtakatifu alinionyeshea Yesu pale msalabani. Alikuwa na njaa, alikuwa na kiu, alikuwa uchi, na alikuwa akihitaji vitu vyote. Kwa nini? Ilibidi iwe hivi kwa sababu alimaliza laana ya umaskini kwa niaba yetu. Alichukua kabisa laana mara moja na kwa wote. Kwa nini? Ili kwamba mimi na wewe, waumini tuliokombolewa kupitia damu ya Yesu, tusipate kuvumilia hiyo nira ya chuma - laana hiyo ya umasikini.
Mabadilishano ya Mungu
Umaskini sio baraka inayotokana na kutii, lakini ni matokeo ya kutotii. Tunamshukuru Mungu, ingawa sisi sote tumekuwa wenye dhambi, Yesu alichukua juu yake mwenyewe uovu wetu sisi sote. Uasi wetu na matokeo yake yote mabaya, pamoja na umaskini, vilikuwa juu ya Yesu alipokuwa akining’inia pale msalabani.
Kubadilishana huku kumefupishwa wazi katika Agano Jipya. Katika 2 Wakorintho tunapata mambo mawili ya kubadilishana katika eneo la vitu. Paulo anasema:
Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri. 2 Wakorintho 8:9
Naye Mungu aweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili katika mambo yote kila wakati, mwe na kila kitu mnachohitaji, ili mweze kushiriki kwa wingi katika kila kazi njema. 2 Wakorintho 9:8
Kuna ubadilishaji gani hapo? Yesu aliuchukua umaskini wetu msalabani ili sisi pia tupate kuufikia utajiri Wake na wingi Wake. Ni kwa njia ya neema. Neema huja tu kupitia Yesu Kristo. Neema haiwezi kuwa mapato. Neema inatokana kwa imani tu.
Katika Kiyunani cha asili, taarifa hiyo katika 2 Wakorintho 9: 8 ni ya kushangaza. Neno kwa wingi linatokea mara mbili, na neno yote linatokea mara tano! Hivi ndivyo Yesu ametupatia. Alimaliza laana ya umaskini ili tupate kurithi baraka.
Baraka katika maeneo yote matatu tuliyopewa na Yesu ya kiroho, ya kimwili na ya vitu zimefupishwa katika mstari huo mzuri wa waraka wa tatu wa Yohana, aya ya 2, ambapo Yohana anasema:
Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu. Huo ni urithi wako kama muumini wa Yesu Kristo.
Koda: TL-L097-100-SWA