Katika barua yangu iliyotangulia, nilieleza kwambatunapokuwa Wakristo, tunajikuta moja kwa moja tukiingiakatika vita vikubwa vya kiroho ambavyo vinavyoeneambinguni na duniani. Zaidi ya hayo, adui zetu wenye nguvuna hatari zaidi ni ufalme wa malaika waovu ambao makao yaomakuu yako katika ulimwengu wa mbingunii.

Kwa hekima na rehema zake Mungu ametupatia silaha zotetunazohitaji ili kupata ushindi. Kwa sababu vita vyetu vikokatika ulimwengu wa kiroho, basi silaha zetu pia ni za kiroho.Katika 2 Wakorintho 10:4 Paulo anasema kwamba “silaha zavita vyetu si za mwili bali zina nguvu katika Mungu hatakuangusha ngome.”

Ngome tunazoshambulia pia ni za kiroho. Kwa karne nyingiShetani amezijenga katika mioyo na akili za wanadamu. Ningome za hofu, tamaa, chuki, ibada ya sanamu, ubaguzi warangi, ushirikina wa kidini na mengine mengi.

Ni ngome hizi zinazokatisha juhudi zote za wanasiasa kujadiliamani ya kweli. Hoja za kimantiki na za kisiasa zinazoungamkono mapatano yaliyojadiliwa hazina nguvu ya kutoshakuvunja ngome za kiroho zinazozuia amani.

Amani ya kweli itakuja duniani tu wakati ufalme wa Kristoutakaposimamishwa hapa. Hili ndilo lengo la vita vyetu kamaWakristo na kusudi la kutumia silaha zetu za kiroho. Nikuvunja ngome za kiroho katika mioyo ya wanaume nawanawake na kuandaa njia kwa ajili ya Kristo kusimamishaufalme Wake—kwanza katika mioyo yao na hatimaye katikadunia nzima.

Silaha Saba za Kiroho

Katika Waefeso 6:13–18 Paulo anaorodhesha silaha saba zakiroho—au vifaa vya kiroho—tunavyohitaji. Anatoa mifanoyake kutoka kwa vifaa vya askari wa Kirumi katika siku zake.Ifuatayo ni orodha hio:

1. Mkanda wa ukweli (Mstari wa 14)

Katika siku za Paulo, wanaume na wanawake kwa kawaidawalivaa mavazi marefu, yaliyolegea ambayo yalifika magotinimwao. Kabla ya kufanya kazi yoyote nzito au shughuliinayohitaji nguvu,jambo la kwanza walilopaswa kufanyalilikuwa ni kukusanya yale mavazi yao marefu na kuyatia ndani ya mkanda wao. Baada ya hapo ndipo waliweza kuwahuru kufanya kazi kwa bidii. Ndiyo maana tunasoma marakadhaa katika Maandiko maneno haya: “Jifungeni viunovyenu.”.

Kutumia mkanda wa ukweli kunamaanisha kuacha kila ainaya udanganyifu au maelewano na uovu. Tukishindwa'kuyakusanya na kuyaweka kando' mambo hayo, yatatuzuiakusonga mbele kiroho. Tunapaswa kuwa waaminifu kwaukweli wa Neno la Mungu hata pale unapokuwa wa utata auhaukubaliki na watu wengi.

Kutumia mkanda wa ukweli kunamaanisha kuacha kila ainaya udanganyifu au maelewano na uovu. Tukishindwakuyakusanya na kuyaweka kando mambo hayo, yatatuzuiakusonga mbele kiroho. Tunapaswa kuwa waaminifu kwaukweli wa Neno la Mungu hata pale unapokuwa wa utata auhaukubaliki na watu wengi.

“Basi wekeni mbali uovu wote, na hila zote, na unafiki,

na husuda, na masingizio yote; kama watoto wachangawaliozaliwa sasa yatamanini maziwa yasiyoghoshwa ya

Neno, ili kwa hilo mpate kuokoka.”1

Zaidi ya yote, tunapaswa kuwa wazi kabisa na wa kwelikatika mahusiano yetu na Mungu Mwenyewe. Hili ni sharti lakupokea ufunuo wa kiroho. Katika Zaburi 51:6 Daudianasema:

“Angalia, wapendezwa na ukweli ulio moyoni, Na katika siriutanijulisha hekima.”

Mungu hudhihirisha hekima yake iliyofichika kwa wale tuwalio na ukweli ndani ya mioyo yao.

2. Dirii ya Haki (mstari wa 14)

Hii hulinda moyo wetu. Katika Mithali 4:23 tunaonywa:

Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo,Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Mafanikio yetu katika maisha ya kiroho yanategemeakudumisha uhusiano mzuri wa moyo na Mungu pamoja namwanadamu. Ni lazima tufuate kielelezo cha Paulo ambayealisema kwamba anajitahidi “kuwa na dhamiri isiyo na lawamambele za Mungu na mbele ya wanadamu sikuzote.”2

Aina ya haki Mungu anayoitazamia si tu kukubali mafundishokwa akili. Ni hali ya moyo, si ya akili.

“Maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki...”3

Wala sio kufuata tu kanuni za kidini. Paulo mwenyewealikuwa amejiweka katika ufuatiliaji wa sheria hizo kwa miakamingi, lakini alipokutana na Kristo, nia yake ikabadilika:

“...ili nimwone Kristo na nionekane ndani Yake, nikiwa

sina haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, baliile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo

kwa Mungu kwa njia ya imani.”4

=== 3. Viatu vya maandalizi ya injili ya amani (aya ya15) ===

Askari wa Kirumi walivalishwa viatu imara sana ambazoziliwapa uwezo mkubwa wa kusafiri haraka. Wangewezakutembea eneo kubwa kwa haraka bila maandalizi ya mudamrefu.

Kama Wakristo, tunahitaji kuwa watu waliotayari kusonga—tukiwa tayari kwa ajili ya makusudi ya Mungu popote nawakati wowote anapotuita, hata bila taarifa ya mapema aukatika hali zisizotarajiwa. Hii inahitaji maandalizi. Tunapaswakufahamu ukweli wa msingi wa Injili na jinsi ya kuieleza kwamtu asiyeamini.

Pia, ni injili ya amani. Tunaweza tu kuiwasilisha kwa ufanisiikiwa tuna amani ya kweli mioyoni mwetu—amani isiyoyumbakutokana na hali za nje. Kwa mwenye dhambi aliye nawasiwasi na kuchanganyikiwa, sauti yetu yenye utulivu naupole inaweza kuwasilisha ujumbe wetu kwa ufanisi zaidikuliko maneno tunayoyazungumza.

4. Ngao ya imani (Mstari wa 16)

Neno lililotafsiriwa hapa kama ngao linahusiana na nenomlango. Urefu wake ulikuwa mkubwa kuliko upana wake.Askari aliyefunzwa vizuri angeweza kuinama na kujikunjakiasi kwamba mwili wake wote ungebaki umefunikwa nakulindwa kabisa. Hata hivyo, alihitaji kuwa mwenye nguvu namwili wenye wepesi; mtu aliyenenepa sana asingewezakujikinga vizuri.

Vivyo hivyo, ngao yetu ya imani lazima iwe kamili katikavipimo vyake vyote. Inapaswa kufunika utu wetu wote—roho,nafsi, na mwili. Tunapaswa pia kuwa tumefunzwa kiroho kiasikwamba tunaweza “kujikusanya” ndani ya eneo lililofunikwakabisa na ahadi za Maandiko Matakatifu. Chochote katikamaisha yetu ambacho ni cha kujipendekeza au kisichohitajikakitabaki nje ya ulinzi wa ngao hiyo.

Wakati mwingine mishale ambayo Shetani hutumia dhidi yetuni “moto.” Mishale hii imewashwa moto, na madhumuni yakesi tu kujeruhi bali pia kuwasha moto wa uharibifu mahaliinapolenga. Inaweza kuchochea moto wa umbea, kashfa, au mgawanyiko ndani ya familia au hata kanisa zima. Lakini ngaoya imani — ikitumiwa kwa uangalifu na kwa ufanisi — si tukwamba itazuia mishale hiyo, bali pia itazima kabisa motowake..

5. Chapeo ya wokovu (Mstari wa 17)

Kama vile dirii inavyolinda moyo wetu, vivyo chapeo yawokovu hulinda akili yetu—mawazo yetu. Akili ni eneoambalo Wakristo wanashambuliwa mara kwa mara. Ndani yaakili zetu mara nyingi kuna vita vinavyoendelea. Shetanihutafuta kuingiza mawazo ambayo yatatuvuruga aukutukengeusha au kutufanya tushindwe kufanya kazi katikavita vyetu dhidi yake.

Mungu amenifundisha mimi binafsi masomo mengi katikaeneo hili. Nilipookoka kwa mara ya kwanza, akili yanguilikuwa inashambuliwa mara kwa mara na huzuni na kukatatamaa. Nilielewa kwamba nilihitaji ulinzi wa kudumu katikaeneo hilo. Niliposoma orodha ya silaha za kiroho katikaWaefeso 6:13–18, niligundua kwamba ilikuwa chapeo yawokovu ambayo nilihitaji. Lakini nilijiuliza: “Najua kwambanimeokoka. Je, hiyo inamaanisha tayari nina chapeo yawokovu, au ni kitu ninachohitaji kupata baada ya wokovu?”

Nilipofikiria jambo hili, nikaona kuwa Wakristo wa Efesoambao Paulo alikuwa akiwandikia tayari walikuwawameokoka. Lakini bado Paulo aliwaagiza wachukuechapeo ya wokovu. Kwa hiyo, ni wazi kwamba nilihitajikufanya vivyo hivyo. Lakini hii chapeo ya wokovu ilikuwa niniambayo inapaswa kuwa ulinzi wa akili yangu?

Kwa bahati nzuri, nilikuwa nikitumia Biblia yenye marejeleotofauti ukingoni. Rejeo kwa Waefeso 6:17 ilikuwa 1Wathesalonike 5:8: “...na tumaini letu la wokovu kamachapeo.” Maandiko hayo yalibadilisha maisha yangu yamawazo. Ikiwa kukata tamaa ilikuwa tatizo langu, basimatumaini ilikuwa suluhisho sahihi.

Nilianza kutafuta—na katika baadhi ya visa nikajifunza kwamoyo—mistari ya Maandiko iliyokuwa msingi wa matumainiimara na ya kudumu. Leo hii, akili yangu inalindwa kwaufanisi!

Nilianza kutafuta—na katika baadhi ya visa nikajifunza kwamoyo—mistari ya Maandiko iliyokuwa msingi wa matumainiimara na ya kudumu. Leo hii, akili yangu inalindwa kwaufanisi!kiroho na kushindwa kuendelea.

Sasa, tuangalie silaha mbili zilizobaki.

=== 6. Upanga wa Roho (Mstari wa 17), ambalo niNeno la Mungu ===

Upanga huu unaweza kutumika kwa ulinzi na pia kwamashambulizi, lakini kimsingi ni silaha ya kushambulia. Mtummoja aliwahi kusema: “Ulinzi bora zaidi ni kushambulia,” namara nyingi hili ni kweli katika ulimwengu wa kiroho.

Neno lililotafsiriwa hapa kama “Neno” ni rhema, likimaanishaneno lililonenwa. Si Biblia iliyo kwenye rafu au mezani ndiyoyenye nguvu, bali ni pale tunapochukua Maandiko Matakatifumdomoni mwetu na kuyatangaza kwa ujasiri kupitia midomoyetu—ndipo yanapogeuka kuwa upanga mkali wenye makalikuwili.

Zaidi ya hayo, Paulo anasema ni “Upanga wa RohoMtakatifu.” Tunaweza kulitumia Neno la Mungu kwa manenoyetu, lakini linakuwa na nguvu kamili pale tu Roho Mtakatifualiye ndani yetu ndiye anayelitumia.

Mfano kamili wa jinsi ya kutumia Upanga wa Rohounaonekana katika tukio la Yesu alipokutana na Shetanijangwani. Mara tatu Shetani alimjaribu Yesu, na kila maraYesu alimshinda kwa maneno yale yale: “Imeandikwa.”5 Yesuhakutumia silaha nyingine ila rhema—neno lililonenwa laMungu. Mungu ametupatia sisi Wakristo silaha hiyo hiyo.

Ni muhimu, hata hivyo, kukumbuka mambo mawili. Kwanza,Yesu alikuwa tayari “amejazwa na Roho Mtakatifu.”6 Ni RohoMtakatifu ndani ya Yesu ambaye alimwongoza katikamatumizi ya upanga.

Pili, Yesu alikuwa amehifadhi Maandiko moyoni Mwake. Kamakijana Myahudi wa wakati wake, alikuwa amekariri vifunguvingi vya Maandiko. Kwa hiyo, alipokabiliwa na Shetani,hakuhitaji kusoma vitabu au kutafuta rejeo—Neno lilikuwatayari ndani Yake!

7. Maombi yote (Mstari wa 18)

Silaha hii ya saba haijaorodheshwa kwa namna ile ile kamazile sita za mwanzo, lakini ni muhimu sana kukamilisha vifaavya askari wa Kikristo. Kati ya silaha sita za awali, Upanga waRoho pekee ndio wa kushambulia na hata huo hufanya kazikadiri mkono wa askari unavyoweza kufika.

Lakini silaha hii ya saba—maombi yote—haina mipaka.Tunaweza kuiita kama kombora la masafa marefu. Maombiyenye umakini, yanayoongozwa na Roho Mtakatifu,yanaweza kufika mabara mengine na kugonga shabaha kwa usahihi kamili. Bila shaka, hii ndiyo silaha yenye nguvu zaidina yenye ufanisi mkubwa katika hazina ya silaha za Kikristo.

Kama ilivyo kwa Upanga wa Roho, maombi yote hupataufanisi wake kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Lazimayaombewe “katika Roho.” Mungu hawezi kukabidhi silahakama hii kwa Wakristo wanaoongozwa na tamaa au hisia zakimwili tu.

Maombi yote yanajumuisha aina nyingi tofauti zamaombi—kama yale yaliyoorodheshwa katika 1 Timotheo 2:1:dua, maombi, maombezi na shukrani. Si sauti ya mtu mmojapekee, bali ni waamini wengi wanaounganishwa kwa umojana Roho Mtakatifu.

Wakati mwingine Mungu huruhusu vikwazo vikubwavinavyoonekana haviwezekani ili kuamsha maombi ya ainahii. Katika Matendo 4:15–18, mitume walikabiliwa na hila yakishetani iliyoweza kusitisha kabisa kazi ya Injili. Baraza laWayahudi, mamlaka ya juu ya kidini, liliamuru rasmi kwamba,mitume “wasiseme kabisa wala wasifundishe katika jina laYesu.”

Wapinzani wa Injili walitambua umuhimu wa kipekee wa Jinala Yesu, kwa kuwa:

“Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote,

kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbinguwalilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa

kwalo.”8

Kwa amri hii ya baraza, Shetani alikuwa amejenga “ngome”ambayo ingezuia maendeleo zaidi ya injili au ukuaji wa kanisachanga.

Lakini waamini wote walikusanyika pamoja kuomba msaadawa Mungu. Wakiwa kama orkesta moja, walimlilia Bwana kwanguvu. Mungu alijibu kwa onyesho la nguvu zake, kwani:“Mahali walipokuwa wamekusanyika pamoja pakatikisika;wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakalinena Neno la Mungukwa ujasiri.”9 Silaha ya maombi yote ilikuwa imebomoangome ya Shetani.

Leo hii, katika sehemu nyingi duniani, Shetani ameundavikwazo na upinzani vinavyozuia maendeleo ya Injili. Njia zakawaida za uinjilisti haziwezi kuvivunja. Ni wakati sasa wakanisa kutumia silaha yake yenye nguvu zaidi — silaha yamaombi yote.

Mada ya barua yangu inayofuata—na ya mwisho—katikamfululizo huu itakuwa Kilele cha Mapambano.

11
Shiriki