Tunapozaliwa mara ya pili kama Wakristo katika ufalme waMungu, tunagundua kwamba tumenaswa katika vita naufalme wa kiroho unaopingana—ufalme wa Shetani. Katikajambo hili hatuna chaguo. Kwa sababu ufalme tunaohusiananao uko vitani, sisi ni sehemu ya vita hivyo. Tunagundua piakwamba tuna aina mbalimbali za maadui, lakini ufalme wenyenguvu zaidi na wa kutisha zaidi ni ufalme wa malaika waasikatika ulimwengu wa roho chini ya utawala wa adui mkuu waMungu, Shetani.

Kwa sababu tuna maadui wenye nguvu kama hao, sotetunahitaji kutumia ulinzi ambao Mungu ametupatia.

Katika 1Wakorintho 11:10 Paulo anaeleza kwamba wanawakeWakristo wanahitaji ulinzi wa mamlaka ya kimaandiko juuyao—inayofananishwa na kifuniko kinachofaa juu ya vichwavyao. Lakini huu ni mfano mmoja tu wa kanuni ambayoinatumika kwa ujumla zaidi kwa Wakristo wote—wanaume na wanawake pia. Kila Mkristo anahitaji ulinzi wa kuwa chini yamamlaka sahihi, ya kimaandiko.

Chini ya Mamlaka

Luka 7:1–10 inarekodi jinsi akida wa Kirumi alivyotuma wazeefulani wa Kiyahudi kwa Yesu kumuomba amponye mtumishiwake, ambaye alikuwa karibu kufa. Yesu alikubali kwenda nakumwombea huyo mtumishi, lakini yule akida akajibu:

“ Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe

kuingia chini ya dari yangu. Ndiyo maana sikujionahata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu,naye mtumishi wangu atapona. Kwa kuwa mimimwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka,nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu,‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia,‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu,

‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”

Kwa kusema “Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwachini ya mamlaka ,” yule akida alitambua kwamba mamlakaya Yesu katika ulimwengu wa kiroho yalikuwa sawa namamlaka aliyokuwa nayo katika eneo la kijeshi kama akidakatika jeshi la Kirumi. Katika hali zote mbili, mamlaka yao yalitokana na kutii chanzo cha mamlaka kilicho juu yao. Kwayule akida, chanzo kilikuwa Mfalme wa Kirumi. Kwa Yesu,chanzo kilikuwa ni Mungu Baba.

Kumbuka, pia, kwamba yule akida hakusema—kama wengiwangefanya—“Nina mamlaka,” bali alisema “niko chini yamamlaka.” Alithibitisha kanuni ya msingi ya Maandiko: ili mtuawe na mamlaka, ni lazima awe chini ya mamlaka. Mamlakadaima hutiririka kutoka juu kwenda chini.

Katika Mathayo 28:18, baada ya kufufuka kwake, Yesualisema:

“Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”

Kuna minyororo ya mamlaka inayoshuka kutoka kwa MunguBaba kupitia Yesu Mwana hadi katika kila hali ulimwenguni.Katika 1 Wakorintho 11:3 Paulo anaeleza kwamba kunamnyororo wa mamlaka unaoshuka ambao umekusudiwakufanya kazi katika kila familia duniani: “Kichwa cha kilamwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke nimwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu. .” Mamlakahushuka kutoka kwa Mungu Baba kupitia Yesu Mwana hadikwa mume na kupitia kwa mume hadi kwa mke.

Lakini kile ambacho ni kweli nyumbani kinatumika kwa kilaidara nyingine ya maisha. Kinawahusu Wakristo wote. KilaMkristo anahitaji ulinzi wa kuwa chini ya mamlaka inayofaa.Mkristo asiye chini ya mamlaka ni Mkristo asiye na ulinzi.

Mamlaka Katika Kanisa

Katika Waefeso 1:22 Paulo anasema kwamba Mungu alimtoaYesu kuwa “kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa.”

Neno la Kiyunani la kanisa ni ekklesia. Katika maana yake yaasili, ekklesia iliashiria kundi la raia katika jimbo la jiji (kamavile Athene) ambao walikuwa serikali ya pamoja ya jiji hilo.Linapotumika kwa Wakristo, linaonyesha kwamba katikamatendo yake ya ukombozi Yesu anatumia mamlaka yakekupitia kanisa ambalo ni ekklesia Yake.

Kuwa chini ya mamlaka ya Kristo, kwa hivyo, inamaanishakuwa na uhusiano sahihi na kanisa Lake. Hatuwezi kudaiulinzi wa mamlaka ya Kristo juu yetu ikiwa hatuheshimumamlaka ambayo ameweka katika kanisa lake.

Hii inaonyeshwa wazi katika uteuzi wa Paulo kama mtume.Katika 1 Timotheo 1:1 Paulo anajiita:

“... mtume wa Kristo Yesu, kwa amri ya MunguMwokozi wetu, na ya Kristo Yesu aliye tumaini letu.”

Mamlaka ya juu kabisa ya utume wa Paulo ilikuwa ni uamuziwa Mungu Baba na Mungu Mwana uliofanyika mbinguni.Lakini kwa maana halisi, “mtume” ni “mtu aliyetumwa.” Utumewa Paulo haukuwa na ufanisi, kwa hivyo, hadi "alipotumwa"kutoka kwa kanisa la mtaa huko Antiokia.

Katika Matendo ya Mitume 13:1, Paulo (ambaye wakati huobado aliitwa Sauli) ametajwa miongoni mwa watu watanowaliokuwa “manabii na walimu.” Kisha, kufuatia maelekezo yaRoho Mtakatifu, wale watu watatu waliobaki waliweka mikonoyao juu ya Barnaba na Sauli na kuwatuma. Baada ya hapo,wote wawili waliitwa mitume (tazama Matendo 14:4, 14).Utume wa Paulo uliamuliwa mbinguni, lakini ulianza kufanyakazi rasmi pale tu ulipotambuliwa na kutekelezwa na kanisa lahapa duniani.

Katika zaidi ya miaka hamsini ya huduma duniani kote, sikuzote nimejitahidi kutambua na kuheshimu mamlaka ya Kristoinayofanya kazi kupitia kanisa la mtaa. Kwanza mimi naLydia—na kisha Ruth na mimi—siku zote tulishirikiana nakutaniko la mahali popote ambapo makao yetu yalikuwa.Tulipotoka katika safari zetu za huduma, tulitumwa rasmikutoka kwa kanisa la mtaa. Tuliporudi, tulitoa ripoti kwakanisa lililotutuma. Hili lilikuwa ni tendo lililoanzishwa naPaulo na Barnaba katika Matendo 13:3 na 14:26–27.

Baadhi ya Wakristo wanatafuta kanisa kamilifu. Lazima nikirikwamba kwa zaidi ya miaka hamsini bado sijapata kanisakama hilo. Lakini basi sina budi kukiri pia kwamba kamaningepata kanisa kama hilo, singeweza kujiunga nalo, kwasababu baada ya kujiunga nalo lingekuwa si kamilifu tena!Wakati huohuo ninashukuru kwa kila kitu kizuri ambachonimepokea kupitia makanisa mbalimbali ya mahali pamojaambayo hayajakamilika.

Washiriki wa Mwili Mmoja

Katika Waefeso 1:22–23 Paulo pia anatoa picha ya pili kuhusuwatu wa Mungu hapa duniani. Anasema “kanisa ambalo nimwili Wake [Kristo].”

Katika 1 Wakorintho 12:27 Paulo anaendeleza mada hii: “Basininyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja pekeyake. Anatumia mifano mbalimbali kutoka kwa mwili wakibinadamu kuonyesha kwamba, kama Wakristo, sotetunategemeana na tunamhitaji kila mmoja wetu.

Maelezo kamili na yenye mamlaka zaidi kuhusu kanisa kamamwili wa Kristo yanapatikana katika kitabu cha Waefeso.Hivyo basi, ni jambo la muhimu zaidi kwamba katika warakahuu wote Paulo anazungumza mara kwa mara juu yaWakristo katika wingi. Kwa hakika hana la kusema kwaWakristo binafsi.

Kwa mfano, katika Waefeso 1:3–12 Paulo anasema yafuatayo:

“Mungu ametubariki—Alituchagua—Alituchagua

mbele—Alitufanya tukubalike—tunaukombozi—Ametujulisha siri ya mapenziYake—tumepata urithi—tunapaswa kuwa kwa sifa. ya

utukufu wake.”

Ukiusoma kwa makini waraka huu wote utaona kwamba huondiyo ujumbe wake kutoka mwanzo hadi mwisho. Hakunaahadi wala maombi yanayolengwa kwa mtu mmoja mmoja. Nikatika mistari sita ya mwisho tu ambapo kuna tofauti ndogo:Paulo anahitimisha kwa kuomba maombi maalum kwa ajiliyake mwenyewe.

Mtazamo huu kuhusu mwili wa Kristo kwa pamoja unafikiakilele chake katika Waefeso 6:10-18 ambapo Pauloanazungumza kuhusu vita vyetu vya kiroho. Katika mstari wa12 maneno yote muhimu yako katika wingi——yakirejeleawatu wa Mungu na pia nguvu zinazopinga: tunapigana nafalme—mamlaka—wakuu—majeshi....

Vita vya kiroho vinavyoonyeshwa hivi si vita kati ya watubinafsi, bali ni vita vikubwa kati ya majeshi yanayopingana.Hakuna nafasi hapa kwa "wapiganaji wa peke yao"wanaofuata malengo yao binafsi. Ushindi utahitaji hatua zapamoja na zilizo na nidhamu kutoka kwa watu wa Munguwakifanya kazi pamoja kama viungo vya mwili mmoja. Hiiitahitaji nidhamu na utayari wa kutii mamlaka ya Kimaandiko.

Katikati ya Uasi Unaoongezeka

Moja ya mambo yaliyokuwa ishara ya mwisho wa wakati huuwa sasa, ambayo Yesu aliwaonya wanafunzi wake, nikuongezeka kwa uasi:

“Na kwa sababu ya kuongezeka kwa maasi, upendowa wengi utapoa.”1

Yesu alionyesha kwamba Wakristo wengi wangeathiriwa nauasi huu unaotawala, na matokeo yake upendo wao kwaMungu na kwa watu wake ungepungua.

Kiini cha uasi ni kukataa mamlaka. Hili limekuwa jambo lawazi katika tamaduni za kisasa. Kuna dharau kubwa kwasheria au kanuni zozote zinazozuia uhuru wa mtu binafsi.Watu wako makini sana kudai “haki” zao, lakini wana uvivumkubwa katika kutambua wajibu wao unaolingana na hizohaki. Wakati mwingine, hali hii hupelekea mazingirayanayokaribia machafuko au kutokua na utawala. KamaWakristo, tunapaswa kujilinda dhidi ya mtazamo wa aina hii.Tunapaswa kuonyesha heshima yetu kwa mamlaka halali za kidunia.

Lakini kabla ya yote, tunapaswa kukuza na kudumishamtazamo wa heshima na utii kwa Mungu Baba yetu na kwaYesu Mwokozi wetu. Hii itaonyeshwa kupitia mtazamo waheshima na utii kwa Neno la Mungu, yaani MaandikoMatakatifu.

Katika Yohana 14:23–24 Yesu alisema:

“Mtu akinipenda, atalishika neno Langu... Yeyeasiyenipenda, hayashiki maneno Yangu.”

Tunaweza kudai kwamba tunampenda Mungu, na tunawezahata kuomba maombi marefu na yenye maneno mazuri aukuhubiri mahubiri marefu yenye mvuto, lakini mwishowehatumheshimu wala kumtii Mungu zaidi ya tunavyoheshimuna kutii Neno lake. Katikati ya hali ya uasi unaotawala, nivyema kila mmoja wetu afanye upya tamko la kujitoakikamilifu na kwa dhati chini ya mamlaka ya Maandiko. “KilaAndiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho.”2

Mahusiano Yetu ya Binafsi

Eneo moja kuu ambalo utii wetu kwa Mungu na Neno Lakeutajaribiwa ni lile la mahusiano yetu ya binafsi. Yesu amewekakanuni kali sana kuhusu jambo hili.

Kuhusu kusamehe watu wengine, kwa mfano, Anasemakatika Marko 11:25–26:

“Nanyi kila msimamapo kusali, sameheni mkiwa na

neno na mtu, ili naye Baba yenu aliye mbinguniawasamehe ninyi makosa yenu. Lakini kama ninyimsiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni

hatawasamehe ninyi makosa yenu.”

Tena, mwishoni mwa ombi la kielelezo ambalo Yesualiwafundisha wanafunzi Wake katika Mathayo 6:9–13,aliongeza maelezo haya:

“Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba

yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Balimsipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu

hatawasamehe ninyi makosa yenu.”

Siku zote tunahitaji kukumbuka kuwa kusamehe mtumwingine si onyesho la hisia bali ni tendo la nidhamu binafsi.Kwa hili tunaweza kumtegemea Roho Mtakatifu, ambaye niRoho wa “nguvu, wa upendo na wa nidhamu.”3

Kujitia nidhamu kunahitajika pia ili kuzaa aina ya mtazamoambao Paulo anaeleza katika Waefeso 5:21: “Nyenyekeanenininyi kwa ninyi kutokana na kumcha Kristo.” Mtazamo huu wakunyenyekea ni ufunguo wa mahusiano sahihi nyumbani nakanisani.

Wakristo wanaokataa kusamehe wengine au kunyenyekeawanakwenda kinyume na Maandiko. Shida yao kuu ni uasi.wamejiweka wazi kwa roho ya uasi inayotawala ulimwenguunaowazunguka. Bila shaka itawafanya wawe hatarini kwamalaika waovu ambao ni adui zao wasiokata tamaa katikaulimwengu wa roho.

== Matakwa Matatu YasiyowezaKupunguzwa ==

Tunakabiliwa na maeneo matatu ambamo Maandikoyanafichua matakwa ya Mungu yaliyo wazi na yasiyowezakupunguzwa, ambayo yanawahusu Wakristo wote. Lakwanza ni heshima kwa mamlaka ya Kristo inayofanya kazindani na kupitia kila kanisa la mtaa. Pili ni msamaha usio namasharti kwa wote waliotukosea au kutudhuru. La tatu nimtazamo wa unyenyekevu na kujinyenyekeza kwa Wakristowenzetu wote.

Utii katika maeneo haya matatu unawapa Wakristo kifunikocha mamlaka ya Kimaandiko kinachowalinda dhidi yamashambulizi ya malaika wa kishetani katika ulimwengu wakiroho. Kinyume chake, kutotii kwao huwafanya Wakristowawe katika hatari ya kushambuliwa na nguvu hizo za giza.

Barua hii imeandikwa kutokana na mzigo wa moyo wakibinafsi. Kwa kuzingatia miaka mingi ya uzoefu katika mwiliwa Kristo, nina hakika kwamba matokeo ya kutotii mashartihaya matatu ya Maandiko yanaweza kuwa ya kusikitishasana. Ninaamini kuwa hili ndilo moja kati ya sababu kuuzinazowafanya watumishi wengi wazuri ,waliojiweka wakfukwa Bwana wameangamia. Ninaomba kwamba Munguatujalie sisi sote heshima mpya kwa mamlaka ya Kristoiliyowekwa katika Kanisa Lake na kwamba afanye upya ndaniya kila mmoja wetu mtazamo wa msamaha na utii.

Katika barua yangu inayofuata nitashughulikia silaha za vitavyetu vya kiroho.

7
Shiriki